Saturday, 14 November 2015

hursday, 16 April 2015

UGAIDI NCHINI KENYA

Matt son sang

Twasikitika moyoni, huenda ikawa aushini,
Serikali jameni, kwani tulichagua nani?
Mhalifu mlangoni, japo hamuoni,                                                         Mwalala kitandani, wananchi mashakani,
Ukuta tutaujenga, iwapo ufa hautazibwa.

Wakenya wasio na hatia, kila mara tunawapoteza,
Wazazi na marafiki wanalia, serikali muwape mwangaza,
Ni lipi serikali mwanuia? Wakenya machungu wanameza,
Hadi lini mhalifu atatuingilia? Wakenya moyoni wajiuliza,
Ukuta tutaujenga, iwapo ufa hautazibwa.

Rais na mawaziri, walinzi wamewazingira,
Mwandishi wa hili shairi, wahalifu wamemzingira,
Ni wakati gani mutakiri, kupuuza huleta madhara?
  Viongozi sio siri, mwafananishwa na “mutura”
Ukuta tutaujenga, iwapo ufa hautazibwa

Siasa mumeipa kipau mbele, waliowachagua mnawapa kisogo,
Bungeni mwapiga kelele, ahadi zenu zageuka uwongo,
Wakenya machozi tele, tamaa kuu kugeuka udongo,
Wakenya twajuta milele, adui wetu mkuu ni hongo
Ukuta tutaujenga, iwapo Ufa hautazibwa

MATHEW KIPSANG at 01:55

Share

 

Sunday, 25 October 2015

Sarah uko wapi??

Sarah moyoni twasikitika, machozi yatiririka,
Moyoni twajiuliza, nani kakupeleka. Chuoni twakumbuka, moyo nzuri wa kutajika, 
Mazuri ukatupa, baraka zako ukatupa. 
Sarah uko wapi, nani kakupeleka?

Kila tunapopumzika, mawazo yatiririka, 
Sura yako ya kutajika, akilini yachoreka. 
Sauti yako yasikika, kila pahali twajipeleka, 
Taswira zako zapangika, kila tunapoamka. 
Sarah uko wapi, nani kakupeleka?

Bidii yako ya mchwa twakumbuka, hadi tutakapopumzika, 
Maanake kupumzika, kila mmoja hutarajia, 
Uhai maulana katupa, vile vile uhai kachukua, 
Sababu kuu ajua, mmojawapo akupenda. 
Sarah uko wapi, nani kakupeleka?

Twatumai kukutana, huko kwake maulana, 
Maanake hii dunia, sio nyumbani hakika, 
Wakati mwema pahali pema, afya njema maisha mema, 
Safiri salama, msalimu maulana. 
Sarah uko wapi ' nani kakupeleka??

RIP DIA SARAH WE LOVE YOU

MATHEW KIPSANG at 23:47

Oh God, you are the most high

God you are the most high.
Whenever I want to cry,
You make me smile.

Every morning I open my eye,
I look at the sky,
Where is the most high?

Your Angels will always fly,
When Satan wants me to cry.
Satan will always lie,
But God, you will always shine.

make me smile and let go the cry
Make me fine and keep me in your file.
Let your light shine for me all the time.
Because you are the most high.